Umeisikia ya Mwanamke wa Mombasa Kumleta Mtoto wa Alikiba? (U-heard)


Leo June 29, 2017 kwenye XXL ya Clouds FM Soudy Brown ametuletea hii inayomhusu mwimbaji staa wa Bongofleva Alikiba anayedaiwa kufuatwa na mwanamke aliyetoka Mombasa Kenya hadi Tanzania akiwa na mtoto anayedai ni wa AliKiba hivyo anahitaji matunzo ya mtoto.

Inadaiwa mwanamke huyo alikutana na Alikiba alipokuwa kwenye show Mombasa na amekuja Tanzania ili kupata haki yake kwa kuwa tangu ajifungue hakuwa na mawasiliano naye.

Soudy Brown alimtafuta Alikiba ili kujua ukweli na majibu yake yalikuwa:

“Dada gani..? Amlete mtoto sasa. Kama kuna mtu anaongea hivyo vitu si unaenda unamuona na unamsikiliza na kama ana mtoto lazima apime damu (DNA).” – Alikiba.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!


Related Posts

Post a Comment