JPM amuamshia Dude Boss wa Tantrade Kwenye Viwanja vya Sabasaba

Katika hotuba yake kwenye maonesho hayo Rais JPM amewaomba waandaaji na viongozi kuweka mipango ili kujenga Hotel na Majengo mapya katika viwanja hivyo akiwataka wajenge kiwanda kitakachowasaidia watanzania kupata ajira na kukarabati majengo kama yamechakaa.

“Haingii akili wao ndio wanatusisitizia mambo ya biashara na viwanda na theme ya mwaka huu inazungumzia kukuza biashara na maendeleo ya viwanda sasa wao badala ya kuzungumza juu ya maendeleo ya viwanda wanataka wajenge Hotel hapa, watengeneze majengo mapya sasa. Sijaelewa.

“Sasa kama hizo hela zipo basi mzipeleke mkajenge kiwanda cha mfano. Haya majengo yaliyopo ambayo mnayaona yamechakaa hawa wanaokuja kuonesha bidhaa zao wapeni bure wajenge ili kila mwaka wawe wanaonesha.

“Hiyo Hotel kwani mkijenga lazima walale hapa hapa? Mnaweza kujenga Hotel hapa bado wakaenda Hotelini mjini. Mimi nilifikiri ili kujenga jenga majengo fikirieni zaidi katika kujenga viwanda kwa ajili ya mfano wa kuonesha Wizara kweli iko mbele kwa kujenga viwanda.

“Haya majumba yanaweza yakawa siyo mazuri sana lakini ni mazuri kwa watu wa Tanzania ambao wanataka kuona bidhaa. Yanayowaleta hapa siyo majumba Watanzania wanakuja hapa kuangalia Tecknolojia na vifaa vilivyomo.

“Inawezekana mimi nipo tofauti mnisamahee lakini katika muelekeo wangu ninaona hizo hela mnataka kuzitumia vibaya. Mwenyekiti nimekuteua juzi umeshaanza kufikiria majengo hapa pamoja na Body yako mnanifanya nifikirie zaidi.

“Nimeshasema, nimewapongeza na ninawapongeza washiriki wote basi tuangalie masuala ambayo ni very positive kwa Taifa hili tunataka kuwa na viwanda vingi na siyo Hoteli nyingi.” Magufuli.

ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!


Related Posts

Post a Comment