BENKI
ya NMB imezindua akaunti mpya kwa wafanyabiashara wadogo na wa kati
ijulikanayo kama 'NMB FANIKIWA ACCOUNT' ili waweze kukua kibiashara
pamoja na kupata maendeleo ya biashara wanazozifanya.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam katika
uzinduzi wa akaunti hiyo ya wafanyabiashara wadogo na wakati, Mkurugenzi
Mtendaji wa Benki hiyo, Ineke Bussemaker, alisema kuwa akaunti hiyo
haina masharti magumu wakati wa kuifungua pamoja na uendeshaji wake
hivyo kuwataka wafanyabiashara wote kuitumia.
Alisema
kuwa NMB imebuni akaunti hiyo kutokana na kuwepo kwa changamoto ya
wafanyabiashara wadogo kukosa mikopo na kukabiliwa na riba kubwa kwenye
mikopo. Akifafanua zaidi juu ya bidhaa hiyo, Mkuu wa Idara ya Biashara,
James Meitaron alisema Benki ya NMB imeweza kufikia kila kundi katika
kuwanufaisha wafanyabiashara wadogo hasa kimikopo ambapo imewanufaisha
katika kuendeleza biashara zao.
Alisema
Benki ya NMB imekuwa ikifanya kazi kwa ukaribu na serikali pamoja na
taasisi zake, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha inawakuza wafanyabiashara
wadogo na wakati wakiwemo 'mama lishe'.
Mkutano huo ukiendelea
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB, Ineke Bussemaker (kulia) akizungumza na mmoja wa wateja wa Benki ya NMB kushoto.
No comments:
Post a Comment