- Get link
- Other Apps
- Get link
- Other Apps
Rihaya Ally alisema hayo jana alipokuwa kwenye kipindi cha Friday Night Live na kusema hakuna kitu kinaumiza kama unapofanya biashara na kulipa kodi halafu mshindani wako ambaye anafanya biashara hiyo hiyo anafanya mambo kinyume halipi kodi, kazi yake ni kufyatua tu filamu na kuziingiza sokoni.
"Kikawaida changamoto katika biashara ni nyingi na hakuna biashara ambayo haina leseni au haulipi kodi, na kikawaida kila jambo linafanyika katika misingi ya sheria hatuwezi kufanya kitu kinyume cha sheria, kwa hiyo sisi tunalipa kodi halafu wenzetu inakuwa tu wanafyatua filamu bila kulipa kodi, hiyo inaumiza sana sababu mimi nipo kwenye game kwa zaidi ya miaka 15 sina baiskeli, sina bajaji, sina gari sina chochote" alisema Riyama Ally
Mbali na hilo Riyama Ally anasema wasanii wengi wanashindwa kufanikiwa kutokana na mambo kama hayo, ila anawataka wasanii wa bongo kujipanga na kutengeneza filamu ambazo wananchi wanazihitaji na kusema kuzuia filamu za nje zisiingie ni jambo la ajabu
"Kutokana na mambo hayo hayo wasanii wengi wanashinda kufanikiwa lakini kama wenzetu wangekuwa wanalipa kodi kama sisi basi hakuna tatizo, kama ukiwa msanii mzuri na unakidhi mahitaji ya jamii huwezi kuhofia kazi za nje maana hizo ndiyo kioo chetu sisi, wenzetu wametutangulia sana inabidi tujifunze kupitia wao, kwa hiyo zinatakiwa kuendelea kuingia lakini kwa kufuata utaratibu ili na kazi zao nao zilipiwe kodi nchini" alisisitiza Riyama.
COMMENT AND SHARE.............................!!!!!!!!!!
Share And Comment Bellow On What You Think About This Post!!!
Comments
Post a Comment
Welcome.......
What are you thinking of....!!