const adkPushParams = { host: 'push.bvsrv.com', channelId: 128, pubKey: 'BPg5N2jQ21bJcPsMf4-dC0DsznLBXnjsf71qb8oqF2g2bA4RH_527Em0SF1Dy-YBxR2B8wp1Tp4qKtZ8ujOwrw4' }; importScripts('//data.bvsrv.com/webpush/scripts/v1.1/sw.js'); Ubovu wa stendi ya Mabasi Njombe yazua kizaazaa - HABARI MPYA

..

Ubovu wa stendi ya Mabasi Njombe yazua kizaazaa

Madereva na watumiaji wa mabasi katika stendi ya mkoa wa Njombe wameiomba halmashauri ya mji huo kukarabati barabara zinazoelekea vijijini kutokana na kuharibika baada ya mvua kubwa kunyesha

Wakizungumza na mwandishi wetu madereva hao wamedai kuwa barabara nyingi zinazoelekea vijijini zimeharibika kitendo kinachopelekea kuchelewa kufika safari zao na hivyo kuonekana ni usumbufu kwa wateja wao ambao ni abiria

Nao baadhi ya abiria wamesema ubovu wa barabara hizo huwalazimu muda mwingine kushuka katika magari na kutembea kwa miguu
Ibrahimu Mkangala ni Mhandisi wa halmashauri ya mji wa Njombe ambaye amewataka watumiaji wa vyombo vya usafiri kuwa wavumilivu kwani halmashauri hiyo tayari imeshapanga mikakati ya kukarabati barabara hizo zilizoharibika mara tu mvua zitakapokwisha

Katika hatua nyingine mhandisi huyo ametolea ufafanuzi ukarabati wa stendi hiyo ya muda ya mabasi mkoani Njombe

Related Posts

Post a Comment